Sehemu ya Kuwepo!
20 Jan
Wanakwenda kwa jina la Offside Trick na kwa sasa naweza kusema kundi hili limeweza kupata umaarufu sana kutokana na wimbo wao wa ‘Samaki’ na ‘Bata’.
Wengi wanaimba je maana yake jamani tunaelewa au tunaimba tu?
20 Jan

Janet Jackson ambaye ni dada wa marehemu MJ,aweka wazi mikakati yake ya mwaka 2010 na kusema kuwa anataka kuwa karibu na Mungu pamoja na kusomea lugha.
Akitoa maelezo yake kwenye gazeti la Gotham la nchini Marekani,Janet adai anataka kuwa karibu na Mungu tofauti na alivyokuwa mwanzo pamoja na kutaka kusomea lugha ambayo mpaka sasa hajajua ni lugha gani kati ya Spanish,French au Italian.
Hata hivyo albam inakuja kutoka kwake ambayo anadai itakuwa ya kihalisia zaidi…
Thats from Janet.
11 Jan

Hiki ni choo cha walimu wa shule ya Msingi Sinza iliyopo jijini Dar es salaam..Toa maoni yako kutokana na picha ya choo hiki...
11 Jan
Ni mmoja kati ya wanaharakati wa Bongo fleva nchini waliopiga kimya kwa uda mrefu bila kujua wako wapi na wanafanya nini..
Hapa namzungumzia Adili Chapakazi niliyebahatika kukutana nae na aliniambia kuwa hayupo kimya kama watu wanavyofikiria kwani kwa sasa amejichimbia pande za Kigamboni kwa ajili ya matayarisho ya filamu mpya aliyoiandaa chini ya lebo yake ya Chapakazi films.
“Sipo kimya kabisa kama watu wanavyofikiria kwani nimegeukia upande mwingine wa sanaa kwakuwa sasa nipo zaidi kwenye upande wa filamu huku hiphop ikiwa bado kwenye damu”Adili.
Filamu hiyo inayoandaliwa na Chapakazi Filmz itabeba jina la Loleza na washiriki mbalimbali kama Mansuli na Buff G watakuwa ndani ya Loleza…Muda ukifika Adili atatueleza wapi tunaweza kuipata Loleza…
11 Jan
Baada ya uzinduzi kufanyika ndani ya ukumbi wa Diamond,sasa albam ipo mtaani na Sugu ameamua kuwapa deal Wamachinga ili waweze kusambaza albam hiyo mtaani….Kama wewe ni mjanja na unahitaji kupata copy ya The hiphop legendary basi piga simu +255 716 62 73 44 .. ili uweze kupata copy yako mkononi!
6 Jan
Hellow guys/fans wa angaliabongo.co.tz…..Nimekuwa kimya kwa kipindi kirefu sana kiasi cha watu kujiuliza nipo wapi na kwanini siweki kitu kwenye gazeti tandu letu hili….
Well majukumu tu fulani yalikuwa yananiweka bussy lakini Nimerudi rasmi kuendeleza kile ambacho wewe umekuwa unahitaji kujua kutoka kwangu….
Ni mwaka mpya hivyo na mambo lazima yatakuwa mapya…Kwa mapenzi ya mwenyezi Mungu tumeweza kumaliza mwaka hivyo naamini atatufanyia yale mema ambyo tutahitaji kutoka kwake…
Special thanks kwa wadau wote wa angaliabongo,Mzee wa Changamoto popote ulipo kwa kuweza kunipa the best Ideas kuhusu angaliabongo,www.bongocelebrity, www.sautizabongo.blogspot.com, shukrani za dhati, The one n only hubby,you know who u r,umekuwa mstari wa mbele kunipa ushauri n all that..Rafiki wote kwa ujumla including Best from Holland, Rama wa UK, wifi Zulfa,got lot of them so hata na wewe ni mmojawapo bila kuisahau family yangu..
THANKS AND HERE WE GO AGAIN!
Always
Sarah!
Una lolote nitumie kupitia
Recent Comments