Sehemu ya Kuwepo!
29 Oct
Sipo na uhakika na hili suala na ndio maana nimeamua kuliweka hapa ili wewe mdau uweze kuweka ukweli…Je hivi ni kweli kwamba wanawake wenye vidole virefu huwa wako Good and Sweet on bed?
29 Oct
Hawa ni wanafunzi wa shule ya msingi moja iliyopo hapa nchini Tanzania.Kuna wabunge husika na kuna serikali lakini bado hali hii ipo,Je kwa wanafunzi hawa karne ya 21 ipo??Serikali naomba ifumbue macho kuhusu hali kama hii.
23 Oct
Wanamuziki kutoka nchini Uganda ambao kwa sas a ndio talk pande zile,Radio na Weasal wamekuwa washindi pekee kutoka Afrika Mashariki kuchukua tuzo yza African Music Awards zilizofanyika nchini Uingereza wiki iliyopita…
Hii imeonesha ni kiasi gani wanamuziki hawa chipukizi walivyoweza kuiteka music industry hapa East Africa..
Wanamuziki wengine waliopata tuzo kutoka Afrika ni pamoja na 2FACE,Dbanj pamoja na Samini.Kwa nchini Ali Kiba alichaguliwa kwenye kinyang’anyiro hiko lakini ameambulia patupu!!!!!

23 Oct
Kuna kisa kimoja nilikisikia sehemu nikaona ni heri niandike kuhusu hili ili na wewe mdau uweze kuelezea kile unachofikiria.Kisa chenyewe ni hivi:
Kuna mama mmoja ana watoto watano ambao kila mtoto na baba yake.
Watoto hao kwa sasa ni wakubwa tu na wamefikia umri wa kujuana vyema na wanahoji inakuaje wamezaliwa mama mmoja na baba tofuati?na kuhisi kuwa mama yao alikuwa hajatulia kwakuwa kila mtoto na baba yake.
Suala hili linawezakana likawa ni kweli kuwa mama wa watoto hawa hakuwa mtulivu kwenye mahusiano yake kutokana na kuwa na kila mtoto na baba yake.
Lakini kuna upande mwingine ambao siku zote sikuwahi kufikiria kabisa kuhusu upande wa mama,unajua ni nini?Kuwa inawezekana mama huyu alikuwa anaingia kwenye mahusiano na baada ya kuzalishwa anakimbiwa au anakutana na wanaume ambao wanamdanganya na kumzalisha,Je ulishawahi kufikiria hivyo?
Cha muhimu tusiwe tunawalaumu wamama/wanawake ambao wamezaa na wanaume tofauti kwakuwa hatujui wamepitia mangapi.Ni hayo tu!!Leta mchango wako Mdau katika hili!

21 Oct

Silvester,Bonge na Ghea Habib ndani ya uwanja wa Kambarage,Shinyanga.

Watu walikesha na Ngwear pia.

Baby Madaha akishow what her mama alichompa.
19 Oct
Wanasiasa 40 walipata ajali mbaya sana porini,na baada ya ajali hiyo alitokea mkulima mmoja na alipoona hivyo alichimba shimo kubwa na kuwazika wote kwa pamoja.
Baadaye polisi walikuja eneo la tukio na kumkuta huyo mkulima na kuanza kumhoji kuhusiana na ajali hiyo pamoja na maiti.
na mahojiano yalikuwa hivi:-
Polisi :- Uliona ajali jinsi ilivyotokea?
Mkulima :- Hapana, nilikuta imeshatokea na maiti zimezagaa..
Polisi :- Zipo wapi maiti?
Mkulima :- Nimezizika
Polisi :- Una uhakika wote walikua wamekufa?
Mkulima :- Kuna wengine walikuwa wanalalamika kwamba hawajafa lakini si unajua wanasiasa walivyo waongo!!!mi nikajua tu wanadanganya nikawazika wote….
18 Oct

Watanzania waishiyo nchini India wanaocheza mpira wa miguu wamefuzu kuingia fainali baada ya kuwafunga Oman bao 2-1.
Ramadhani Mwanga anayejulikana zaidi kama Ramadinho aliiwezesha timu yake ya Tanzania kujipatia ushindi na hivyo kufuzu kuingia nusu fainali watakaocheza na Germany.
Kila la kheri Watanzania nchini India
15 Oct
Ni mmoja kati ya waanzilishi wa Bongo fleva nchini na hapa namzungumzia Sugu ambaye wiki iliyopita ameachia wimbo ‘Hold On’ aliomshirikisha Andre ambao umeanza kufanya vizuri kwenye radio mbalimbali nchini….
Wimbo huo upo kwenye albam mpya ya SUgu inayotarajiwa kuzinduliwa mwezi Dec itakayokuwa na jumla ya nyimbo kumi..
Hii ni kwa ufupi tu ILA kwa zaidi endelea kuAngaliabongo!
15 Oct
Alizaliwa tarehe 13 April,Same as my birthdate but different years na alifariki siku ya tarehe 14 Oct 99′..
Miaka yote hiyo amekuwa akisimama kuona kuwa Tanzania inakuwa nchi ya kujitegemea yenyewe na hilo alifanikiwa kwa njia moja au nyingine.
Tutamkumbuka kwa mengi lakini kubwa zaidi ambalo alilifanya hayati baba wa Taifa ni kuhakikisha TZ inakuwa nchi ya amani na hilo tunaliona..
Mungu amlinde Hayati baba wa Taifa..
15 Oct
SAMAHANI SANA KWA KUTOKUWA HEWANI NA HILO LILITOKANA NA MATATIZO YA KIUFUNDI…SASA TUENDELEE PAMOJA!Angaliabongo,Sehemu ya kuwa!
ASANTE
SARAH.
Recent Comments