Ni kitu kipya ndani ya Angalia Bongo..Kila siku ya Ijumaa nitakuwa nakuletea maana ya maneno ya mitaaani yanayoongelewa sana siku hizi na vijana..Kwa wiki hii naanza na maneno haya

Umefulia-Umeishiwa kifedha.
Gambe-Pombe.
Kicheche-Mwanamke/mwanaume malaya.
Mzigo-Kitu chochote kizuri/mwanamke
Mwamwi(mwanzo mwisho)-Hakuna kuachia jambo fulani mpaka ieleweke.
Related posts:

Hiyo “kufulia” ndio imekuwa so “in” mpaka basi…lol
Kwani weye Candy! umefulia? Lol
Usiogope kuambiwa umefulia kwani pengine asemaye ndiye asiyejua kuwa amefulia na ndio maana badala ya kukosoa anabaki kufurahia makosa ama maishio ya wenzake.
Ni kama kusimama katikati ya barabara ukasaula bila aibu ukidhani hawakuoni kumbe wewe ndiye uliyefumba macho.
Hahahahahaaaaaaaaaaa. Labda na maoni yangu yamefulia.
Thanx Sarp. Tutavinjari hapa Ijumaas kupata yale ya kitaani
Blessings