Sehemu ya Kuwepo!
28 Aug
Ni kitu kipya ndani ya Angalia Bongo..Kila siku ya Ijumaa nitakuwa nakuletea maana ya maneno ya mitaaani yanayoongelewa sana siku hizi na vijana..Kwa wiki hii naanza na maneno haya

Umefulia-Umeishiwa kifedha.
Gambe-Pombe.
Kicheche-Mwanamke/mwanaume malaya.
Mzigo-Kitu chochote kizuri/mwanamke
Mwamwi(mwanzo mwisho)-Hakuna kuachia jambo fulani mpaka ieleweke.
28 Aug

Kipaji kipya from Young Money, Drake aachia ngoma yake ingine inayokwenda kwa jina la ‘Forever’ aliyowakutanisha wakali wa Hiphop,Kanye,Em pamoja na Wizzle…Kabla ngoma hii haijaachiwa leo hii,ilikuwa tayari imesha-leak kupitia internet…
28 Aug

Besta ambaye aliwahi kutamba na ngoma ‘Baby Boy kutoka nchhini akana kuwa na mimba ya Marlaw na kuweka wazi kuwa hata uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki huyo hana zaidi ya kuwa majirani tu.
“Sina ujauzito wa Marlaw,nashangaa imesambaa hivyo,Marlaw ni jirani yangu na rafiki mkubwa lakini si zaidi ya hapo”Besta.
Aliongezea kuwa ana mpenzi wake na Marlaw ana mpenzi wake hivyo watu waelewe hilo..
28 Aug
msanii spark ajitoa tip top connection,spark amedai kinachomkimbiza kwenye chama hilo ni mkwanja mbuzi anaoupata ukilinganisha na kazi anazopiga,spark amedai kuwa uongozi unakula ela nyingi kuliko yeye anyepiga ngoma kali na hivyo kufikia hatua ya kujitoa,mkubwa wa kundi alidakwa na camera yetu na kusema kama ifuatavyo,unajua wasanii wengine hawana akili,wanapokuja kuomba udhamini wanakuja wakiwa na adabu na heshma kwa kuwa wanakua hawana kitu hivyo uongozi hutumia ela nyingi kuwalipia ku record na pia videos lakini mwisho wa siku wanapoanza kupata majina wanasahau walikotoka nakuanza kuvimba kichwa na kudai ela haitoshi,wametoka wengi kama akina mb dog cassim,z anto pingu na desso na spark pia lakini chama wala halitoshuka chini ni ma speed yaleyale,
27 Aug

Wanamuziki P-Squere kutoka nchini Nigeria wanatarajia kutoka na muonekano mpya pamoja na kuachia albam yao nyingine ya ‘Danger’ inayotarajia kutoka mwezi ujao.
Peter na Paul walihabarisha kuwa wana muonekano huo mpya utaonekana siku ambayo wataachia albam hiyo hivyo watu waae tayari kwa New P-Squere LOOK of the year 2009.
24 Aug

Anatamba na ‘Problem‘ ngoma iliyomuweka juu more than ever..Ni Cpwaa ambaye mwenyewe anadhibitisha kuwa ameleta mabadiliko kwenye muziki wa Bongo kwa kutambulisha Bongo Crank na watu kuweza kumkubali.
Kubwa zaidi kutoka kwa Cpwaa ni ile staili yake ya kuweza kujua habari zake kupitia simu yako ya mkononi ambayo ameitambulisha siku zilizopita kidogo.
Lengo hilo kubwa la Cp la kuweza kupata habari zake kupitia simu yako ya kiganjani limekuja kutokana na yeye mwenyewe kuwa mtu wa kupenda kutumia sana Technolojia.
Anadai kuwa amesomea Technology hivyo hana budi kuitumia…..Anaachia ngoma mpya kabla ya mfungo wa Ramadhani na baada ya hapo kuna kitu maalumu kakuatayarishia wewe fan wake…anadai ni kiteknolojia zaidi…Nini hiko?Endelea kuangalia Bongo….Utaelewa tu!
24 Aug

Baada ya kusemwa sana kuwa amemuiga mwanamuziki mwenzake Rihanna ile style ya nywele na hair stylishh wake kumtetea kuwa style ile ilikuwa ni kwaajili ya kipindi hiki cha summer,Ciara aamua kulivua wigi na kurudia style aliyozoeleka na watu.
Kama unavyomuona pichani akiwa na long hair na kufunga midomo ya wale waliokuwa wanaamini kuwa kakata nywele kumuiga Rihanna.Hapo alikuwa kwenye event iliyoandaliwa na Lucacris Foundation huko
Malibu, Los Angeles juzi.
24 Aug

Wiki iliyopita wasanii hawa kutoka Tiptop Connection walitangaza rasmi kujitoa kundini humo kwa kudai ni sababu binafsi..Baada ya muda kidogo,Tunda akasema kuwa hajajitoa na aliyejitoa ni Spark.
Story inaendelea kwa Tunda kumpiga biti Spark kutoimba wimbo walioimba pamoja wa ‘Ripoti Mtaani’ kwakuwa wimbo huo aliutunga Tunda na ni mali ya Tip Top Con.
Spark anamwambia kuwa ataimba kwakuwa wimbo huo alitoa idea yeye na kujitoa kundini n sababu binafsi hivyo asimzingue…Sasa kieleweke kipi kati ya hawa wasanii tokea TipTop Conn?Ni utoto au?
www.angaliabongo.co.tz itakuletea zaidi kitakachotokea baina ya wanamuziki hawa wawili
23 Aug

Pichani ni baadhi ya washiriki wa filamu ya Baby Powder
Baby Powder filamu mpya kabisa ya Kibongo itakayoachiwa mapema tarehe 26 mwezi wa kumi na moja iliyochezwa nchini Marekani.
Filamu hii itahusu maisha halisi ya watanzania waishio nchini Marekani.Kwa kifupi tu kuhusu filamu hii ni Mtanzania alimaliza elimu yake huko Kansas na kwenda kuamua kutafuta kazi mji mwingine.
Akiwa mji mwingine wa Atlanta,anajiunga na watu wengine ambao wana maadili mabaya.Kijana huyo anataka kujaribu kujitoa na hapo ndipo panakuwa na kazi kwani inakuwa TOO LATE…Ni moja ya filamu bora ambayo hutakiwi kukosa kuinunua.
23 Aug

Simu zinauzwa,Black Berry 8990 pamoja na G1.Kwa maelezo zaidi wasiliana na Festo Faustine,Namba za simu ni +255 764 47 18 00.
Recent Comments