Nipo fiti…Banza Stone!

banza

Banza Stone mwana wa Masanja achonga na Angaliabongo na kudai kuwa yupo fiti na atarudi hivyo mashabiki wake wasichoke kumsubiri. Haya ni maswali mafupi aliyohojiwa na Angaliabongo.

Angaliabongo: Banza mashabiki wako wanakuuliza upo wapi na unafanya nini?

Banza: Nipo ila kuna mambo fulani yalikuwa yananiweka vibaya ila siku si nyingi nitaweza kusikika tena na mashabiki wangu.

Angaliabongo: Vipi madai ya kuwa unaumwa na uzushi wa kifo?

Banza: Kwakweli ndio maana naitwa Makaveli kwakuwa kila siku nazushiwa kifo lakini kama unavyoniona,mimi ni mzima wa afya njema.

Angaliabongo: Banza unasumbuliwa na nini hasa kwasababu tunaona tu kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuwa unaumwa,nini hasa kinachokusumbua?

Banza: Nasumbuliwa na kichwa pamoja na malaria na si kinginecho.

Angaliabongo: Je mashabiki wako wategemee nini kutoka kwako?

Banza: Wategemee kitu special,nitatoa wimbo maalumu kwa wale wote wanaonisema vibaya.

Angaliabongo: Asante Banza

Banza: Asante!

Share and Enjoy:
  • Print
  • Digg
  • MySpace
  • Twitter
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Google Bookmarks
  • Reddit
  • Technorati

Related posts:

  1. Banza abambwa live na simu ya wizi
  2. Ni wakati wa albam-Maunda
  3. Nipo Single na nimerudi mzigoni-Ray C
  4. Bado Nipo Nipo V/S Ndoa Haina Doa….
  5. Kwa wavaaji Grillz..Onyo.

About the Author