
Mashindano ya urembo ya kumsaka kisura wa kitongoji cha Kigamboni 2009 kupitia Kampuni ya Bongo5 Media Group,imefikia ukingoni kwakuwa mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika siku ya jumamosi ya May 30 kwenye ukumbi wa Maeese Beach Resort zamani Hunters beach Kigamboni.Washiriki mbalimbali wamejitokeza kushiriki mashindano hayo na mpaka sasa jumla ya walimbwende 11 watachuana vikali kuliwania taji hilo la Miss Kigamboni 2009,aidha katika mashindano hayo burudani itapambwa na THT Odama band,Mwasiti,Maunda Zorro,Barnabas pamoja na Pipi.
Related posts:
