Angalia Bongo

Sehemu ya Kuwepo!

Archive for May, 2009

New Home..Clouds Fm


From Mjengoni Kitega Uchumi to Makazi Mapya…Mikocheni…People’s Station!

  • 2 Comments
  • Filed under: Angalia Bongo
  • Miss Kigamboni Ukingoni!


    Mashindano ya urembo ya kumsaka kisura wa kitongoji cha Kigamboni 2009 kupitia Kampuni ya Bongo5 Media Group,imefikia ukingoni kwakuwa mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika siku ya jumamosi ya May 30 kwenye ukumbi wa Maeese Beach Resort zamani Hunters beach Kigamboni.Washiriki mbalimbali wamejitokeza kushiriki mashindano hayo na mpaka sasa jumla ya walimbwende 11 watachuana vikali kuliwania taji hilo la Miss Kigamboni 2009,aidha katika mashindano hayo burudani itapambwa na THT Odama band,Mwasiti,Maunda Zorro,Barnabas pamoja na Pipi.

  • 0 Comments
  • Filed under: Angalia Bongo

  • Kwa jina anakwenda kama Nurdin ila wengi wanamfahamu kama Scheta au Soulja Boy wa Bongo..Huyu ni msanii chipukizi kabisa anayetamba na ngoma ya ‘Wadhifa’ aliomshirikisha Noorah na Richard…Anasema anamzimia sana Soulja Boy na ndiyo maaana muonekano wake upo kama Soulja Boy Tell Em……..Mpango wake wa baadaye ni kufikia anga za kimataifa na kuweza kufanya ngoma na Soulja Boy.

  • 0 Comments
  • Filed under: Angalia Bongo

  • Hii ilikuwa ndani ya kichwa changu na nimeamua kukiweka hapa ili wadau muweze kushare na mimi mtazamo huu juu ya wasanii wetu wa hapa nyumbani.
    Inasikitisha sana kuona msanii anakuwa kama maji yani kupwa na kujaa,Unajua namaanisha nini?Kuna kipindi unakuta msanii flani anatamba sana kwenye redio,magazeti na kila sehemu kutokana na single yake ambayo imepokelewa vizuri na jamii na kuweza kupendwa lakini baada ya muda jina la msanii huyo linafifia hata msanii mwenyewe kupoteza dira kabisa….HII INATOKANA NA NINI?
    Kwa mtazamo wangu,wasanii wajihusishe na shughuli mbalimbali za jamii ambazo nafikiri zingeweza ku-maintain majina yao kwenye jamii yetu na kuachana na pombe,uzinzi na madawa ya kulevya..
    Kwa mfano halisi…mastaa kibao na wengi wao wa nje mbali na kuimba au kucheza movie wana kuwa na kitu fulani ambacho kina-maintain jina lake kwenye jamii na watu wanapata kumsikia…
    Jay Z pichani alikuja nchini kama balozi wa maji,kama sikosei na alienda Mwananyamala Hospitali kuzindua kisima cha maji safi..Tumeweza kuona Kelly Rowland kama balozi wa Ukimwi na alizuru nchini na kuzama mpaka Uwanja wa fisi,Yvonne Chakachaka kutoka nchini Afrika Kusini kama balozi wa Malaria,Anjela Jolie anahusika na mambo ya UNICEF na wengine wengi tu lakini kwanini wasanii wetu nchini hawafikirii kuhusu hilo na wanaishia kusema Game ya Bongo imejaa ushirikina na maovu mengine na wakati ukweli unaonekana kwamba wenyewe hawajishughulishi?Inasikitisha sana….Ushauri kwa wasanii wote ambao ni wa bure kabisa,wafikirie kufanya kitu fulani katika jamii ambacho kitaweza kuweka majina yao on Top…
    Hongera kwa Moracka ambaye yeye pamoja na gazeti la Bang alijitolea kwenda kwenye vituo vya watoto yatima na kutoa misaada mbalimbali……Kwangu mimi naona nimelifikisha mezani,wadau changieni mtazamo huu

  • 2 Comments
  • Filed under: Angalia Bongo

  • Ujumbe from MwanaFA,kupata kila kitu kuhusu yeye nenda
    www.binamu13.com

  • 0 Comments
  • Filed under: Angalia Bongo
  • Baba Levo na Rich 1 pamoja


    Wasanii wawili waliokuwa ndnai ya TMK …Rich One, na Baba Levo…wameamua kutoka kivyao na albam ya pamoja waliyoipa jina la KAMAKAWA.
    Taarifa kutoka kitaa cha TMK….albam hiyo yenye nyimbo 8… imefanywa katika studio tofauti tofauti ambazo ni Bongo Records chini ya P.Funk, Fish Crub chini ya Producer Lamar na Tongwa Rec chini ya Producer Duke.

  • 0 Comments
  • Filed under: Angalia Bongo
  • wanaume kazini


    kundi la wanaume tmk family lililo chini ya usimamizi wa said fella lime release nyimbo mpya inayokwenda kwa jina la wanaume kazini ambayo inafanya vizuri katika media nyingi za bongo,mkubwa fella hata ivyo alidai kuwa huo ni mwanzo tu kwani kuna project inayokuja initwa mtaa kwa mtaa ambapo wanaume watakua wanpita kila mtaa tanzania nzima wakifanya show zao,na pia kuna pamba zenye nembo yao zinakaribia kutoka soon so washabiki wa wanaume tmk kaeni mkao wa kula nadhani mnamjua mkubwa fella hakisema kitu inakuaje tusubiri tuone

  • 1 Comment
  • Filed under: Angalia Bongo

  • mwanadafada ray c ameibuka na kusema kuwa habari za uzushi zilizoenea mitaani kuwa wameachana ni uongo mtupu kwani wanatarajia kufunga ndo hapo mapema mwakani,ray c alisema piaanatarajia kuacha music ili ajishugulishe na biashara zake nyingine kwani ameona music industry ya kibongo iko na mizinguo kibao hivyo soon ataachana na mambo ya music na kufanya shughuli zake binafsi,kila la kheri lord eyez na rehema chalamila

  • 0 Comments
  • Filed under: Angalia Bongo
  • hili ndio shimo lenyewe jamani,


    wadau hiki ndio chanzo cha habari,kwa style hii imani za kishirikina zinawezekana kabisa zikawa zinatumika,shimo hili na gari alilokua nalo mhehimiwa naamini unaweza pita hata na speed 120 na gari ikatingishika tu,wadau hii ndio bongo dar es salaam,ridhiki ya mtu mikononi kwa mtu,tuatafika kweli

  • 1 Comment
  • Filed under: Angalia Bongo

  • mbunge wa kyela mheshimiwa H.Mwakyembe hatimaye apata nafuu baada ya kupata ajali maeneo ya iringa akiwa na gari lake binafsi,mwakyembe alisema ajali hiyo ilisababishwa na shimo dogo lililopo barabarani ambapo kimuonekano ni dhahiri haliwezi kusababisha ajali mbaya kiasi kile,mheshimiwa alisema ni mbinu tu za wapinzani kutaka kummaliza lakini kwa rekhma za mnyaaz mungu leo yu hai,hivi kweli imani za kishirikina zinaaminiwa hata na wasomi?wadau nipeni jibu

  • 0 Comments
  • Filed under: Angalia Bongo
  • About Angalia Bongo

    Hey how you doing DEAR fan! Thanks for passing By in my world...I would apreciate İf you can call me SARAH, was born in the middle of 80’s.. By proffesion a journalist and always straight with my desicions, without forgeting İ enjoy life to the fullest and always believe in Jesus, Remember İm a pure Christian.Love friends and believe to DİE with something as İ was born with NOTHİNG…İ think thats to much to know about me. Thanks for passing by xoxox..... Read More

    Have Your Say

    How Is our Website?

    View Results

    Loading ... Loading ...

    GrooveBack



    Disco bora na la kijanja nchini, pekee linalowahusisha waliokuwapo, waliopo na wanaotaka kujua kilichotokea